Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Matumizi ya Kitunguu Saumu huboresha Afya

DAR ES SALAAM

Na Joyce Sudi

Kitunguu saumu ni moja ya kiungo chenye ufanisi  mkubwa mwilini katika kuboresha afya ya mwili, Kiungo hiki huwa ni sehemu ya vyakula mbalimbali tunavyokula kila siku, vikiwemo vile vinavyoliwa vibichi kama vile kachumbari na saladi, pamoja na vyakula vilivyookwa au kuchemshwa.
Kwa mujibu wa Taasisi ya Chakula na Lishe Nchini Tanazania {TFN}, kitunguu saumu kina viondoa sumu {antioxidant} ambazo huondoa alkali huru {freeradicals} katika mwili, na hivyo kusaidia kuzuia uharibifu wa sumu hizo mwilini, na pia kina vitamini na madini mengi kwa afya ya mwili, ambayo ni madini ya manganese, calcium, phosphorus, selenium na vitamin B6 na C.
Kitunguu saumu ni moja wapo ya viungo ambavyo mara nyingi hutumika kuongeza ladha katika chakula, ambapo vipo vitunguu saumu vya rangi nyeupe ambavyo huwa na tumba kubwa chache, lakini vipo vyenye rangi ya zambarau au pinki, ambavyo huwa na tumba ndogo na nyingi, ingawa vitunguu hivyo vyote vina ubora sawa.
Licha ya kitunguu saumu kuwa maarufu kutumika kama kiungo, lakini pia hufaa kutumika kusaidia katika matatizo mbalimbali ya kiafya, kama vile kuzuia maambukizi yatokanayo na bakteria, baadhi ya virusi na fangasi, hasa katika utumbo, mapafu na sehemu za ukeni.
Vilevile husaidia katika uyeyushaji wa chakula, kuzuia kuhara na maambukizi yatokanayo na fangasi kwenye kinywa kutokana na viambata vinavyopatikana kwenye vitunguu saumu ambavyo ni; Allicin, Vitamini C, Vitamin B6 na Manganese.
Nini husababisha harufu kali mdomoni baada ya kula kitunguu saumu?
Watu wengi wamekuwa wakisumbuliwa na swali hili, kwamba pamoja na virutubisho na madini muhimu yaliyopo kwenye kitunguu saumu, lakini inakuwa ngumu kutafuna kwa kuhofia harufu kali.
Ukweli ni kwamba pale unapotafuna kitunguu saumu,kemikali za kibaiolojia zilizopo kwenye mfumo wa chakula kwa ajili ya kuvunjwa vunjwa kwa chakula kiweze  kufyonzwa vizuri, hubadilisha kiambata kilichopo kwenye kiungo hicho kiitwacho Allin kuwa Allicin na kisha kuvunjwa zaidi kuwa Ally Methyl sulfide, na hivyo kusababisha harufu kali  ambapo njia  rahisi ya kuepusha harufu hii, ni kunywa maziwa (fresh)yasiyoganda ya ng’ombe.
Taasisi ya Chakula na Lishe Nchini Tanzania {TFN}, imetuandalia  namna ya  kuandaa kitunguu saumu kwa ajili ya kusaidia kutuliza vidonda vya kooni kwa watu wenye maambukizi ya  Virusi vya Ukimwi {H.I.V}.
Mahitaji:
Kitunguu saumu tumba 4, maji kikombe kimoja, na sukari au asali.
Namna ya kuandaa:
i.Menya  maganda kwa kisu na katakata kitunguu saumu.
ii. Tia  kwenye maji yanayochemka, acha kichemke kwa dakika 10.
iii. Ipua, funika na acha ipoe, Kisha ongeza asali au sukari kwa ajili ya ladha.
Matumizi:
Kunywa kikombe kimoja kutwa mara tatu.
Pia kitunguu saumu kinaweza kutumika kama dawa ya kikohozi
Namna ya kuandaa:
i. Ponda kitunguu saumu kilichomenywa maganda .
ii. Weka kwenye kijiko cha chai, chukua kijiko cha chai cha asali au sukari.
Tumia mara mbili kwa siku kwa kikohozi.
Angalizo:
Matumizi ya vitunguu saumu yanaweza kuingiliana na ufanyaji kazi wa dawa mbalimbali za hospital, hivyo hakikisha unamuuliza daktari wako kama hujaanza kutumia kitunguu saumu kama dawa. Pia kwa wale wenye presha usitumie, kwanza pata ushauri wa daktari.
Dawa hizo ni kama Isoniazid ambazo zinatumika kutibu maradhi ya kifua kikuu, cyclosporine, dawa hizi hutumika kwa waliopandikizwa kiungo mfano figo, Dawa za H.I.V. ambapo  kitunguu saumu kinaingiliana na ufyonzaji wa dawa hizi, na hivyo kupelekea dawa kutokufanya kazi.
Pia, Nonsteroidal anti-inflamatory drugs {NSAIDs], dawa hizi ni kama ibrufen, na Naproxen ambazo zikitumiwa pamoja na kitunguu saumu, huongeza kuvuja kwa damu.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.