Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Uinjilishaji katika nchi za Maghreb

Papa Yohane Paulo II Papa Yohane Paulo II

Katika safu hii ya Chimba Chimba Historia ya Kanisa wiki iliyopita, tuliawaletea mada ya historia ya jinsi Uinjilishaji ulivyoingia nchi za Ethiopia, Eritrea na Somalia. Leo tunaendelea na historia ya Uinjilishaji katika nchi za Maghreb.. Sasa endelea…

Katika Kiarabu, nchi za Magharibi mwa Misri huitwa ‘Maghreb’. Nchi hizi ni pamoja na Libya, Tunisia, Algeria na Morroco. Zamani nchi hizi, hasa kwenye mwambao, zilikuwa za Kikristu hadi zilipotekwa na Waislamu katika karne ya saba. Pole pole Ukristo uligandamizwa na kupotea.
Ufaransa iliteka Algiers mwaka 1830 na kufanya Algeria nzima koloni lake, baadaye waliteka Tunisia mwaka 1881 na Morocco mwaka 1912. Libya ilitekwa na Waitaliani mwaka 1912 na kuipoteza kwa Waigereza wakati wa Vita Vikuu vya Pili, mwaka 1942.
Wakati wa ukoloni, Wakristo walikuwa na uhuru wa kuinjilisha, na waliongezeka hadi kufikia milioni moja na nusu. Hata hivyo, hawakuwa na mafanikio makubwa kati ya Waarabu Waislamu. Wengi wa waumini wao walikuwa Wazungu waliohamia kule.
Waarabu walioongoka hawakuzidi 10,000. Utume katika nchi hizo ulifanywa hasa na Wamisionari wa Afrika (Mapadre Weupe) waliokuwa na Makao Makuu yao kule Algiers, Algeria.
Utume wao mkubwa ulikuwa utume wa kuwepo kwa kuonyesha mfano na kufanya matendo mema. Walianzisha vyuo vya kujifunza lugha ya Kiarabu na Uislamu kwa wageni.
Mmisionari mwingine alikuwa Charles de Foucard aliyeanzisha Mabruda na Masista Wadogo wa Yesu. Wao wanajaribu kuishi katikati ya watu na kufanya kazi pamoja nao katika viwanda na sehemu nyingine.
Nchi za Maghreb zilipopata uhuru wake, Wazungu karibu wote bila kungoja kufukuzwa, walirudi Ulaya. Kadri siku zilivyopita, nchi hizi ziliweka sheria ngumu ya kuwabana Wakristo, na hivyo hata Wakristo Waarabu walikimbilia Ulaya na kufanya kazi huko. Hivyo katika nchi za Maghreb hadi leo, Ukristo ni kama haupo.
MOROCCO
Morocco ilipata uhuru wake bila matatizo mwaka 1956. Ingawa iliwekwa sheria ya kukataza Waislamu kuongoka kuwa Wakristo, uhusiano na Kanisa ulibaki mzuri. Tangu mwaka 1952 kuna monasteri ya Wabenediktini inayoendesha semina hasa juu ya Mahusiano ya Dini mbalimbali. Kati ya wakazi milioni 31, Wakristo ni asilimia 0.5, na Wakatoliki ni asilimia 0.2 tu.
ALGERIA
Algeria ilipata uhuru wake mwaka 1962 baada ya vita vikali vilivyodumu miaka 8. Kwa sababu wakati wa vita, Askofu Mkatoliki Etienne Duval alitetea haki za wazawa, baada ya uhuru Kanisa liliheshimiwa.
Hata hivyo, Wakatoliki 800,000 waliondoka wakabaki 80,000 tu. Ila, Mapadre na Watawa walibaki kuwahudumia watu bila ubaguzi. Kati ya wakazi milioni 34, Wakristo ni asilimia 0.9 na Wakatoliki ni asilimia 0.6 tu. Kuna majimbo manne, Mapadre 62 na Watawa wanawake 116.
TUNISIA
Tunisia ilipopata uhuru mwaka 1956, kwa makubaliano kati ya serikali ya Kiislamu na Wamisionari wa Afrika, alama na mambo mengi ya Kikristo katika mji wa Tunis yaliondolewa.
Kwa mfano, sanamu ya mwanzilishi wa shirika iliyokuwa katikati ya mji, ilipelekwa makaburini, Cathedral nzuri ilifanywa makumbusho, kati ya makanisa sabini, sitini na tano yalipewa kwa serikali kwa matumizi ya umma, hata na cheo cha Askofu Mkuu cha Kartago kilishushwa na kuwa Usimamizi wa Kitume.
Hata hivyo, waliimarisha urafiki na Rais wa Tunisia, Bourguiba, ambaye alianzisha uhusiano wa kibalozi na Vatikano. Wamisionari walibaki na chuo chao cha kufundisha Kiarabu kilicholeta mahusiano mazuri. Kati ya wakazi milioni 10, Wakristo ni asilimia 0.3 na Wakatoliki ni asilimia 0.2 tu. Mwaka 1996 Papa Yohane Paulo II (1978-2005), alitembelea Tunisia kuwatia moyo.
LIBYA
Libya ilipata uhuru wake mwaka 1951 kutoka kwa Waitaliani. Baada ya uhuru, idadi ya Wakatoliki ilishuka hadi kubakia 5,000 tu, na baadaye Wamisionari walifukuzwa, Wakopti nao walibakia wachache.
Baada ya mapinduzi ya Kanali Ghadafi, katika makubaliano na Vatikano, Kanisa lilibakiza kanisa moja tu kule Tripoli. Ila baadaye Gadafi aliwaalika Masista manesi kwenda kusaidia watu wake. Hata Masista Watanzania wa Shirika la Konsolata walikwenda huko. Kati ya wakazi milioni 5.4, Wakristo ni asilimia 2.1,   na Wakatoliki ni asilimia 0.3 tu.
Ingawa katika nchi nyingi za Maghreb kuna uhusiano wa kidiplomasia na Vatikano, hakuna uhuru wa kuabudu. Haiwezekani kujenga kanisa au kuhubiri dini kwa Waarabu Waislamu. Kwa Mwarabu kuongoka na kuwa Mkristo, ni kosa linaloadhibiwa kisheria, mahali pengine hata kuuawa.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.