Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Alazimishwa kuoa ili kuasili mtoto, Wakurya wamkaribisha

MWANZA

Na Paul Mabuga

Upepo unavuma katika jua la saa nane, na miti iliyo karibu inatoa ukinzani,  hali hii inazalisha mvumo ulio sawa na wimbo mzuri unaopigwa kwa ala tupu! Hakika, hali hii ingeweza kuwa ya kufurahisha, lakini la hasha! Aron Malifweda [48], [siyo jina lake halisi kwa sababu za kitaaluma], zaidi ya kutafakari kila swali analoulizwa kwa ajili ya makala haya, huku akiwa ameketi kiambazani kwenye nyumba yake iliyo kwenye moja ya miji mdogo kanda ziwa, ni kama haoni wala kusikia kingine cha ziada katika mazingira yake.
Ni kwa sababu amechanganyikiwa na kuzama katika fikra zisizo na msaada wala  ufumbuzi, anaona ni kama ametengwa na jamii yake kutokana na hali aliyonayo, anachokitamani anaona kama ananyimwa, na hivyo kukata tamaa.
Alitaka awe na  watoto, ikashindikana kwa nguvu za kiume [syo rijali]. Lakini sasa anataka kuasili mtoto anakayerithi mali zake, lakini amepewa sharti, kwamba ni  lazima aoe na kuishi na mke.
“Unajua nimehangaika kwa  miaka mingi, iwe kwa madaktari hospitali, ama tiba asilia, lakini sikufanikiwa. Baadaye daktari mmoja ninayemwamini akaniambia kwamba siwezi kuondokana na hali hiyo nilipata huzuni sana siku hiyo, na nikaona dunia yote imeniangukia.
Nikifikira maisha ya kukaa bila mke wala watoto, nilikiona hata kifo kinaninyemelea! Nimehangaika hivii kwa zaidi ya miaka 15,” anasema Malifwedha, wakati akisimulia kisa chake cha sharti la kuhifadhiwa utambulisho.
Anasema kuwa kama suluhisho katika hilo, alishauriwa na daktari huyo kwamba atafute mtoto wa kuasili ndiye atakayekuwa  mrithi wa mali zake, jambo ambalo anaeleza kuwa  awali lilikuwa gumu, kwani wapo waliomkatisha tamaa kwa kumtishia kuwa anaweza kupata kijana, akamlea, lakini baadaye atakapokua, asimjali na kumkimbia akirejea katika familia yake ya uzao wa kibayolojia.
“Walikuwa wananiambia, Unaweza kupata mtoto wa kuasili na kumsomesha, lakini akifika chuo kikuu, akakukumbia na kukutelekeza,” anasimulia Malifwedha na kuongeza kuwa, “Baada ya ushauri wa Maafisa Ustawi wa Jamii katika eneo langu, nilipata moyo wa kuanza mchakato wa kupata mtoto wa kuasili, ambao. Licha ya jambo kwenda vyema, lakini sasa nimefikia pahala umekwama kutokana na sharti nililopewa, kwamba ni lazima nioe!”
Kwa mujibu wa Tovuti ya Wakala wa Uzazi na Vifo, kuasili watoto ni mchakato wa kisheria ambao huhamisha uwajibikaji wa mzazi kutoka kwa wazazi wa kuzaliwa kwa watoto, kwenda kwa wazazi  wa kuwalea. Kuasili mtoto kunaongozwa na sheria  ya kuasili mtoto, Sura Namba 335 Toleo la Mwaka 2002.
Na kwa mujibu wa sheria hiyo, mara mtoto anapoasiliwa, basi unajengwa uhusiano wa kudumu na wa moja kwa maoja kati yake na wazazi waliomuasili, na kwamba haki zote kutoka kwa wazazi wake wa kibayolojia [wa damu] zinafutika na kuhamia katika familia yake mpya. Pia, Wazazi wa damu nao haki zao kwa mtoto aliyeailiwa, nazo zinakoma.
Tukirejea kwa Malifedha, anaeleza kuwa baada ya kupata mtoto wa kuasili, na wazazi wake wa damu kutoa ridhaa chini ya usimamizi wa Maafisa Ustawi wa Jamii, na uchumguzi wa kina kufanyika katika kipindi cha miezi sita, alijaza fomu mbali mbali na taarifa za ufuatiliaji zikaandikwa, tena zikionesha kwamba ana mwenendo mzuri, na ana uwezo wa kuasili.
Bila shaka mchakato kama huu, kulingana na taratibu, baadaye ulihitaji idhinisho la mamlaka ya juu ya Ustawi wa Jamii. Kutoka hapo, hoja hupelekwa mahakamani mbele ya jaji, na  kama kutakuwa na kukidhi matakwa ya kisheria, basi, hutolewa amri ya kuasili, na mchakato huwa umekamilika. Hata hivyo, katika muda wote Maafisa Ustawi wa Jamii huendelea kufuatilia ustawi na maslahi ya mtoto.
Pengine kilichoonekana kuwa ni kikwazo kwa Malifwedha kwa mujibu wa sheria hiyo, ni kwamba mzazi wa kiume anayeishi pake yake haruhusiwi kumuasili mtoto wa kike, ama vingunevyo kuwe na mazingira mahsusi! Ingawaje hata huvyo  anaruhusiwa kuasili mtoto wake wa kiume. Na pia, kuwe na tofauti ya umri wa miaka  isiyopungua 21 kati ya mzazi anayeasili, na mtoto anayeasiliwa.
Tena basi, inaelekezwa katika kanuni za sheria hiyo kwamba katika mazingita yanayofaa, mtoto aliyeasiliwa, atakapofikisha umri wa miaka 14, ataelezwa hali ya kuasiliwa kwake na maafisa ustawi wa jamii katika eneo husika.
Kuhusu suala na kuoa Malifwedha anasema, “Nilikwenda kwa wanasheria, wakaniambia kuwa huyo mwanamke nikimuoa, atakuwa na haki zote kama mke kwenye mali zangu, hata kama itakuwa ni ndoa ya kudanganyia ili tu nipate kibali cha kuasili! Hilo nalo nkaliona gumu. Nikashauriwa niende kwa Wakurya,  eti huko ukioa mwanamke aliyezalia nyumbani, na ukishatioa mahari, watoto wanakuwa mali yako.”
Sadick Hunga ambaye ni Mwandishi wa Habari anayefanya kazi zake Mkoani Mara, na ambaye ni mmoja wa wanajumuia ya Wakurya wanaoishi Mkoani humo,  anasema katika mahojiano kwa njia ya simu kwamba, mila hiyo ipo katika jamii yake na imeendelea kuwepo, kwamba katika jamii hiyo, wakati wote watoto huwa ni mali ya mwanaume aliyelipa mahari.
“Huyu jamaa sisi tunamuambia karibu ‘tata’ [baba]! Yaani huku kwetu, kama mwanamke amezalia nyumbani, akaja mwanaume kumuoa, analipa mahali ya mke, mathalani ng’ombe sita, lakini baadaye atatakuwa kuwalipia watoto mahari nyingine inayoitwa ‘kuborora’, ambayo inaweza kufikia hadi ng’ombe wawili kwa kila mtoto, na kutokea hapo watoto hao wanakuwa mali yake daima dumu, hata wana umri mkubwa namna gani,” anasema Hunga.
Katika mtazamo mwingine Hunga anasema kuwa miongoni mwa jamii ya Wakurya, ikiwa mwanamke ameachana na mume wake, na  ikatokea akaolewa na mwanaume mwingine, basi, watoto wote watakaozaliwa katika familia mpya ni mali ya yule mume wa awali, “na hii imetokea majuzi huko Serengeti! Itaondoka tu ikiwa mume mpya atalipa mahari kurejesha iliyokwishakulipwa kabla.”
Wakati hali ikiwa hivi, Malifwedha bado yupo njia panda juu ya nini akifanye ili kukabiliana na hali hii, kwani ana malalamikio mengine. Anadai kwamba ndugu zake wanamtenga na hususan yanapokuja matukio kama harusi huwa hashirikishwi, na hilo linamuongezea mawazo! “Yaani utasikia tu kuna harusi huko, lakini hushirikishwi, huwa najiuliza, sijui wananionaje,” anasema.
Kuna changamoto nyingine pia, kwani Malifwedha akifikisha umri wa miaka 50, yaani katika kipindi cha miaka miwili ijayo, kwani suala la kuasili litakuwa na kipingamizi, kwani halitakuwa katika maslahi ya mtoto, na hususani katika maendeleo na makuzi yake. Na itakuwa ni kazi kubwa kujenga hoja dhidi ya pingamizi kama hizi kulingana na kanuni za kuasili.
Mrumbi wa masuala ya ndoa na muendeshaji wa kipindi cha ‘Ndoa Aminifu’ cha Runinga ya Tumaini, Paschal Maziku, anasema kwamba ndoa katika Kanisa Katoliki huwa ni kwa ajili ya manufaa ya wanandoa wenyewe, watoto wanaowalea na jamii kwa ujumla, na wala siyo kwa manufaa binafsi kama ilivyo katika jambo hili katika makala haya.
“Isitoshe, huyu bwana hawezi kuwa na ndoa, kwani ndoa huwa kati ya mwanamke na mwanaume rijali. Sasa jamaa na hali aliyonayo, haiwezekani, maana ndoa ili  ikamilike inahitaji kuwa ‘consummated’ [tendo la ndoa kufanyika ndani ya muda unaovumilia kwa busara ana kupatilizwa], kinyume na hapo inavunjwa”
Kuhusu, kuasili watoto, Maziku anasema, huko ni sawa na mtoto kuwa ‘displaced’ [kuwa pasipostahili],  na kwamba, “ni vema tukarejea katika mila zetu, kama ni yatima ama ana mazingira magumu, basi ndugu wa karibu, wajomba, mathalani baba wadogo na wengine, wachukue majukumu yao.”

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.